Monday, May 27, 2013

WAANDAMANAJI WAPINGA NDOA YA JINSIA MOJA UFARANSA

Mamia ya maelfu ya wananchi wa Ufaransa walifanya maandamano makubwa mjini Paris hapo jana wakipinga kupitishwa sheria mpya ya ndoa ya watu wa jinsia moja nchini humo. Waandamanaji hao wameonyesha hasira zao kwa kupinga kitendo hicho cha kinyama kinachokinzana na maadili ya mwanadamu na kuitaka serikali ya nchi hiyo iitengue mara moja. Waandamanaji wameahidi kuendelea kutoa mashinikizo yao hadi pale serikali ya Rais Francois Hollande itakaposalimu amri. Wanaharakati wa kijamii wameeleza kuwa, watu wanaokaribia milioni moja wameshiriki kwenye maandamano hayo ya amani yanayopinga kupitishwa sheria ya ndoa ya watu wa jinsia moja ambayo imeanza kutekelezwa tokea wiki iliyopita. Inafaa kuashiria hapa kuwa, siku chache zilizopita mwandishi mmoja wa Kifaransa alijinyonga Kanisani nchini Ufaransa akipinga kupitishwa sheria hiyo nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO