Monday, May 27, 2013

JESHI LA SUDAN LAANGAMIZA WAASI 70

Jeshi la Sudan limetangaza kuwa, kwa akali waasi 70 wameangamizwa katika eneo la al Dandaro lililoko katika jimbo la Kordofan Kusini. Kanali al Sawarmy Khalid Saad Msemaji wa jeshi la Sudan amesema kuwa, kundi hilo la waasi likitumia silaha nzito kama vile vifaru na mizinga lilivamia eneo la al Dandaro lililoko katika jimbo hilo kwa shabaha ya kulidhibiti, lakini lilikumbana na upinzani mkali kutoka kwa majeshi ya serikali ya Khartoum. Kanali Khalid Saad ameongeza kuwa, kwenye mapigano hayo waasi wasiopungua 70 waliuawa na wengine kukimbia baada ya kuzidiwa nguvu na majeshi ya serikali ya Sudan. Amesema kuwa, majeshi ya serikali yamefanikiwa kukamata ngawira za vifaru viwili aina ya T55 na zana nyingine za kijeshi za waasi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO