Monday, May 27, 2013

SERBIA NA KOSOVO WARIDHIA MAHUSIANO

Umoja wa Ulaya leo umekaribisha idhini ya uhakika iliyotolewa na Serbia na Kosovo kurudisha uhusiano wao katika hali ya kawaida na kusema kwamba hiyo ni hatua moja mbele katika juhudi za kujiunga na Umoja wa Ulaya.
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja huo, Catherine Ashton, amesema anakaribisha uamuzi wa nchi hizo mbili kuupitisha mpango wa utekelezaji ambao unatafsiri kwa vitendo vifungu vya makubaliano waliofikia hapo mwezi wa Aprili. Serikali ya Kosovo iliuidhinisha kwa haraka mpango huo wa utekelezaji baada ya Waziri Mkuu wa Serbia, Ivica Dacic, na mwenzake wa Kosovo, Hashim Thaci, kuufafanuwa hapo Jumatano. Serikali ya Serbia hadi jana usiku ilikuwa ikiutafakari kwa kutaka hakikisho kwamba idhini ya kuutekeleza mpango huo wenye nia ya kurudisha maisha yaliyochafuliwa kutokana na mzozo huko Kosovo hapo mwaka 1999 katika hali ya kawaida, haitomaanisha kwamba serikali hiyo inatambuwa uhuru wa jimbo lake hilo lililojitenga.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO