Monday, May 27, 2013

WAFANYABIASHARA WA JORDAN WASUSIA KIKAO NA UJUMBE WA ISRAEL

Wafanyabiashara wa Jordan wamesusa na kutoka nje ya kikao cha Jukwaa la Kimataifa la Uchumi 'Davos' nchini Jordan, mara baada ya kuingia kwenye kikao hicho ujumbe wa utawala wa Kizayuni. Hatua ya wafanyabiashara wa Jordan inaonyesha msimamo wa nchi hiyo wa kulalamikia vitendo vinavyoyadhalilisha matukufu ya Kiislamu vinavyofanywa na utawala huo ghasibu. Wiki iliyopita, serikali ya Jordan ilimfukuza balozi wa utawala wa Israel mjini Amman ikilalamikia hatua ya kuvunjiwa heshima Masjidul Aqswa, kibla cha kwanza cha Waislamu. Serikali ya Jordan ilichukua hatua hiyo baada ya wabunge wa nchi hiyo kutoa mashinikizo makubwa ya kuitaka serikali imfukuze balozi wa utawala wa Israel nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO