Thursday, May 30, 2013

KIONGOZI WA TALIBAN PAKISTAN ARIPOTIWA KUUAWA NAO WACHAGUA KIONGOZI MPYA

Kiongozi nambari mbili wa kundi la Taliban nchini Pakistan Waliur Rahman ameuawa katika mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za Marekani katika eneo la Waziristan. Maafisa Usalama wa Pakistan wametangaza kuwa, Waliur Rahman ambaye Marekani ilitangaza zawadi ya dola milioni 5 kwa kichwa chake, ameuawa pamoja na wafuasi wake wasiopungua watano baada ya makombora mawili kulenga nyumba yake mapema hapo jana.
Hata hivyo msemaji wa kundi la Taliban amekanusha taarifa hizo na kusema kuwa si za kweli. Kundi la Taliban la Pakistan ni kundi tofauti lakini lenye mfungamano na kundi la Taliban wa Afghanistan na linajulikana kwa jina la Tahreek-e- Taliban Pakistan (TTP). Kundi hilo limefanya mashambulizi mengi dhidi ya jeshi la Pakistan na raia wasio na hatia nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO