Thursday, May 30, 2013

MAKAAZI MAPYA YA WALOWEZI YATATIZA AMANI PALESTINA

Mpatanishi mkuu wa Palestina Saeb Erakat amesema kuwa uamuzi wa Israel wa kujenga makaazi mapya ya walowezi wa kiyahudi mashariki mwa Jerusalem unaharibu juhudi za Marekani za kufufua mazungumzo ya kutafuta amani kati ya nchi hizo mbili.Erakat amesema wanauchukulia uamuzi huo wa Israel wa kujenga makaazi mengine 1,000 kama hatua ya kuhujumu juhudi za waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry.Matamshi ya Erakat yanawadia saa chache baada ya shirika lisilokuwa la serikali kuliambia shirika la habari la AFP kuwa Israel inapanga kujenga makaazi zaidi mjini Jerusalem huku Marekani ikijizatiti kuyafufua mazungumzo yaliyokwama kati ya Palestina na Israel.Ujenzi huo wa makaazi ya walowezi umekuwa ndilo suala  tete lililosababisha kufeli kwa mazungumzo mwaka 2010 na wapalestina wameapa kutorejea katika meza ya mazungumzo iwapo Israeli itaendelea kujenga katika ardhi yao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO