Thursday, May 30, 2013

WAPINZANI SYRIA KUTOSHIRIKI MAZUNGUMZO YA AMANI

Muungano wa kitaifa wa upinzani Syria umesema hautashiriki katika mazungumzo yanayoandaliwa kwa pamoja na Urusi na Marekani huku washirika wa utawala wa Rais wa Syria Bashar al Assad ukijihusisha katika vita kwa kulisaidia jeshi la serikali.Kaimu kiongozi wa muungano huo  George Sabra amewaambia waandishi habari mjini Istanbul Uturuki kuwa muungano huo hautashiriki katika mkutano wowote wa kimataifa au katika juhudi zozote za amani iwapo wapiganaji kutoka Iran na wa kundi la wanamgambo la Hezbollah kutoka Lebanon wataendelea kuivamia Syria.
Wakati huo huo waasi wameomba msaada wa klijeshi na madawa katika mji wa mpakani wa Qusair ambako mapigano makali na majeshi ya serikali yanaendelea. Msemaji wa waasi amesema kuna majeruhi 700 mjini humo.Majeshi ya Assad yanasemekana yanasonga mbele kuuteka mji wa Qusair wakisaidiwa na wapiganaji wa Hezbollah kutoka Lebanon.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO