Thursday, May 30, 2013

VIRUSI VIPYA VILIVYOGUNDULIKA VYAZIDI KUUWA WATU MASHARIKI YA KATI

Taarifa zilizotolewa na shirika la afya duniani (WHO) zinasema kuwa wagonjwa 27 kati ya 49 waliogundulika na virusi hivyo, wameshafariki dunia. Sirika hilo sasa limetangaza kuwa virusi hivyo ni hatari kwa dunia kwani vinazidi kusambaa hivyo nchi zinatakiwa kuwa makini hasa kwa wasafiri wanaotembelea baadhi ya nchi za kiarabu kama Saudi Arabia, Falme za Kiarabu (UAE), Jordan na Qatar. Pia baadhi ya wagonjwa wamepatikana Ufaransa, Tunisia, Uingereza na Ujerumani. Vifo vya hivi karibuni vimetokea mashariki mwa nchi ya Saudi Arabia ambapo watu watatu wamefariki kutokana na virusi hivyo. Pia mgonjwa mmoja alifariki dunia huko Ufaransa baada ya kutokea Mashariki ya kati. Wataalamu wanadai virusi hivyo sio SARS (Severe Acute Respiratory Syndrome) bali ni virusi vipya ambavyo wao wamevipa jina la MERS-CoV (Middle East Respiratory Syndrome Coronavirus). Dalili za ugonjwa huo ni pamoja na kuhisi baridi kali ambayo inapelekea kupata nimonia na pia figo kutofanya kazi ipasavyo. Shirika hilo la afya limomba wataalamu wote duniani kushirikiana nao na kufanya utafiti wa hali ya juu ili kuweza kuzuia virusi hivi visiendelee kuenea na kusababisha vifo vya watu wengi duniani. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO