Thursday, May 30, 2013

WAGOMBEA URAIS IRAN KUANZA MDAHALO KESHO

Mdahalo wa kwanza wa televisheni kati ya wagombea wanane wa duru ya 11 uchaguzi wa rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran utafanyika kesho Ijumaa na kurushwa hewani moja kwa moja na kanali ya kwanza ya televisheni. Mdahalo huo wa kwanza utafanyika saa 10 jioni kwa majira ya hapa nchini na kuwashirikisha wagombea wote wanane wa kiti cha urais. Mdahalo huo utarushwa hewani tena saa tatu usiku hapo kesho katika kanali ya nne ya televisheni. Mbalo na mdahalo wa kesho, wagombea katika uchaguzi wa rais wa Iran watachuana tena katika midahalo mingine miwili itakayofanyika siku ya Jumatano ya tarehe 5 na siku ya Ijumaa ya tarehe 7 Juni. Duru ya 11 ya uchaguzi wa rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran pamoja na uchaguzi wa nne wa mabaraza ya Kiislamu ya miji na vijiji zitafanyika kwa wakati mmoja siku ya Ijumaa ya tarehe 14 Juni

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO