Thursday, May 30, 2013

WHO YATAKA KUPIGWA MARUFUKU MATANGAZO YA SIGARA

Shirika la Afya Duniani WHO limetaka mataifa yote duniani kupiga marufuku matangazo yote ya biashara ya tumbaku kama njia mojawapo ya kupunguza idadi ya wavutaji wapya wa tumbaku. Katika taarifa, WHO inasema kuwa nchi ambazo tayari zimetekeleza marufuku ya matangazo na udhamini kwa bidhaa za tumbaku zimeshuhudia kupungua kwa matumizi ya tumbaku kwa asilimia saba. Nchi ambazo zimepiga marufuku matangazo ya bidhaa za tumbaku ni pamoja na Australia, Canada, Finland, Ireland, Nepal, New Zealand, Norway, Palau na Panama. Kabla ya maadhimisho ya siku ya kupinga matumzi ya tumbaku duniani ambayo ni tarehe 31 mwezi huu, WHO inasema kuwa sekta ya tumbaku inatafuta mbinu tofauti za kulenga wavutaji sigara kupitia mitandao ya mawasiliano au kwa kutumia wafanyikazi wa makampuni ya tumbaku wanaojifanya kuwa wavutaji sigara. Dr Douglas Bettcher mkurugenzi katika idara ya kuzuia magonjwa yasiyoambukiza kwenye Shirika la WHO amesema marufuku kwa aina  zote za matanagazo na udhamini  ni moja ya njia kuu ya kupunguza matumizi ya tumbaku. Amesema watumiaji wengi wa tumbaku huanaza kuitumia kabla ya kutimia miaka 20 na hakuna shaka kuwa sigara ni mada inayoua na kwamba njia pekee ni kupigwa marufuku matangazo yote ya biashara na udhamini wa bidhaa hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO