Thursday, June 27, 2013

JESHI LA NIGERIA LAKAMATA VIONGOZI WA BOKO HARAM

Msemaji wa Jeshi la Nigeria amethibitisha taarifa za kutiwa mbaroni viongozi kadhaa waandamizi wa kundi la Boko Haram katika maeneo ya kaskazini mwa Nigeria. Brigedia Chris Olukolade amesema leo kuwa, licha ya kutiwa mbaroni vinara waandamizi wa kundi hilo, jeshi la Nigeria limefanikiwa kugundua ghala la silaha mbalimbali la kundi hilo. Brigedia Olukolade ameongeza kuwa, miongoni mwa silaha na zana za kijeshi zilizokamatwa na jeshi la nchi hiyo ni maroketi ya aina mbalimbali, mada za milipuko, zana za mawasiliano na laptop kadhaa.
Msemaji wa jeshi la Nigeria amesema kuwa, tokea mwezi Mei mwaka huu, kikosi maalumu kimewekwa katika majimbo ya Borno na Yobe kaskazini mwa Nigeria na kimefanikiwa kuziangamiza kambi kadhaa za kundi hilo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO