Wednesday, June 26, 2013

KIKOSI CHA UN KUANZA KAZI MALI JULAI MOSI

Kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa kitaanza operesheni zake nchini Mali ifikapo Julai Mosi mwaka huu baada ya Baraza la Usalama la umoja huo kutoa kibali hapo jana kwa kikosi hicho.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lenye nchi wanachama 15 mwezi Aprili liliafiki kutumwa kikosi hicho cha askari jeshi 12,600 kinachojulikana kwa jina la Minusma.
Wanajeshi wa Ufaransa watakisaidia kikosi hicho cha Umoja wa Mataifa katika kupambana na waasi wa kaskazini mwa Mali iwapo itahitajika. Ufaransa ikisaidiwa na wanajeshi elfu mbili wa Chad ilianzisha uvamizi wa kijeshi huko Mali kwa kile ilichokitaja kuwa mapambano ya kuwatokomeza waasi wa kaskazini mwa Mali.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO