Wednesday, June 26, 2013

RAIS OBAMA AELEKEA AFRIKA

Rais Barack Obama hii leo anaelekea barani Afrika katika ziara iiliyosubiriwa kwa muda mrefu. Hata hivyo ziara hiyo imegubikwa na suala la hali mbaya ya afya ya kiongozi wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. Ziara hiyo ya wiki moja itamfikisha rais Obama nchini Senegal, Afrika Kusini na Tanzania. Ikulu ya Marekani imesema itashauriana na familia ya Mandela kuona ikiwa rais Obama anaweza kumtembelea mwanasiasa huyo mkongwe aliyelazwa katika hospitali ya mjini Pretoria kwa muda wa wiki tatu sasa. Mandela na Obama hawajawahi kukutana ana kwa ana tangu rais huyo wa Marekani alipochaguliwa kuingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO