Friday, June 28, 2013

RAIS WA SENEGAL APINGANA NA OBAMA KUHUSU USHOGA NA HAKI ZAO

Rais Macky Sall wa Senegal amesema nchi yake haiko tayari kuruhusu ushoga na maingiliano ya ngono kati ya watu wenye jinsia moja. Sall aliyasema hayo jana akijibu matamshi ya mgeni wake Rais Barack Obama wa Marekani aliyezitaka nchi za Kiafrika ziwape mashoga alichokiita haki sawa na makundi mengine ya kijamii. Rais Macky Sall amemjibu Obama akisema: Japo Senegal imeonyesha ustahamilivu mkubwa lakini haiko tayari kuruhusu maingiliano ya ngono kati ya watu wenye jinsia moja.
Obama alikuwa amezitaka nchi za Afrika kuwapa mabaradhuli haki sawa na makundi mengine ya kijamii bila ya kujali mbari, dini na jinsia zao.
Nchi nyingi za Afrika zinatambua maingiliano ya kingono kati ya watu wenye jinsia moja kuwa ni kosa la jinai.
katika miaka ya hivi karibuni nchi kama Burundi na Sudan Kusini zimepasisha sheria zinaotambua maingiliano kama hayo kuwa ni kosa la jinai na nchi kama Uganda, Nigeria na Liberia zinafanya mikakati ya kupasisha sheria zinazozidisha adhabu kwa wale wanaofanya vitendo hivyo vichafu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO