Sunday, July 28, 2013

SUDAN YATAKA MSAAADA KUHUSU WAASI

Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Sudan katika Umoja wa Mataifa ameitaka jamii ya kimataifa iyalazimishe makundi ya waasi ya Darfur kukaa katika meza moja ya mazungumzo na serikali ya Khartoum. Daffa Allah Alial-Haj ameitaka jamii ya kimataifa iisaidie nchi yake katika mchakato wa kurejesha amani na utulivu katika jimbo la Darfur. Amesema, ili kufikia lengo hilo, jamii ya kimataifa inapaswa kuyalazimisha makundi ya waasi yasitishe vitendo vya utumiaji mabavu na kukaa katika meza moja ya mazungumzo na serikali ya Sudan. Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Sudan katika Umoja wa Mataifa amesema, serikali ya Khartoum inaendelea na juhudi zake za kuyakalisha katika meza moja ya mazungumzo makundi ya waasi lakini jamii ya kimataifa inapaswa kuisaidia nchi yake katika hilo. Jimbo la Dafur lililoko magharibi mwa Sudan limekuwa likikabiliwa na hali ya mchafukoge tangu mwaka 2003.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO