Sunday, July 28, 2013

HIZBULLAH YACHELEA UGAIDI NCHI ZA KIISLAM

Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imesema kuwa, ina wasi wasi juu ya kuenea ugaidi katika nchi za Kiislamu.  Sayyid Ibrahim al-Amin, Mkuu wa Baraza la Kisiasa la Hizbullah ya Lebanon ametahadharisha kwamba, tishio la ugaidi Palestina, Lebanon, Iraq, Libya, Syria na Misri linatia wasi wasi na hadi sasa watu wengi wameuawa na wengine kubaki bila makazi kutokana na vitendo vya ugaidi katika nchi hizo. Afisa huyo mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Hizbullah ya Lebanon ameashiria jinai za Wazayuni huko Palestina na vitendo vya kinyama vinavyofanywa na magaidi huko Syria na kuhoji kwamba, kwa nini madola yanayodai kuwa vinara wa kutetea haki za binadamu ulimwenguni yamenyamazia kimya mauaji haya? Mkuu wa Baraza la Kisiasa la Hizbullah ya Lebanon amesema bayana kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel ndio adui mkuu wa Lebanon na muqawama wa wananchi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO